Wito ni wake Bi Nzigire Biringanine, Kiongozi wa avenue Kamagema ya pili pa Panzi ; ujumbe uliyo tolewa hii siku ya sita, tariki 1 Novemba mwaka huu.
Wakati wa kikao kilicho endeshwa katika avenue hiyo asubuyi Kuamkiya, Wakaaji wa eneo hiyo, pamoja na Kiongozi wao, wamekusudiya kuchambuwa hali za usalama katika eneo yao, mizozo kati ya raiya na viongozi, na kutowa pamoja suluhisho, kwa ajili ya kuweza ku boresha hali na kukuza ushirika wa kila Mkaaji kwa kwazi za Maendeleo ambazo ni salongo, kujilindiya usalama na kutowa malalamiko kwa muda unao faa.
Bi Nzigire Biringanine ameshukuru Wakaaji wote waliyo shiriki kwenye kikao hicho, akiwaalika kujiunga pamoja, kwa kuweza kuendesha pamoja Maendeleo ya mungini kwa mafaa ya Wakaaji wote.
Uyu amealika zaidi vijana wa avenue yake kujiunga pamoja kwa ajili ya kulinda usalama wa avenue yao, akilaumu tabiya Mbalimbali ambazo sizo alali kwa Maendeleo ya mungini; huku akiwaomba piya kuepukana na kila watu wanao tafuta kuangamiza Wakaaji wote.
Nao washiriki kwenye kikao hicho wame mshukuru Kiongozi Nzigire Biringanine kwa kusudiyo hilo, wakimuomba piya, yeye pamoja na viongozi wengine wa Panzi kujiunga pamoja ili kutowa suluhisho imara kwa shida za kila aina ambazo ni chanzo cha magonvi kati ya raiya, na kukuza malalamiko ya vijana wa mahali.
Tukumbushe kuwa, kikao hicho kiliweza kuwakusanya Wakaaji zaidi ya 100 wa avenue Kamagema ya pili.























