Mara tu baada ya kusikia kwa mshangao na masikitiko makubwa juu ya msiba huu uliomnyang’anya maisha daktari kijana, Ofisi ya Uratibu ya Mkoa ya Jamii Mpya ya Kiraia ya Kongo, mkoa wa Kivu Kusini, imetoa msimamo wake wa kulaani vikali tukio hilo na imetaka maelezo ya wazi, ya kweli na yasiyopingika ili ukweli kuhusu sababu na mazingira ya kifo hicho iweze kujulikana.
Ofisi ya Uratibu imelifafanua tukio hili kuwa ni matokeo ya wivu na ushindani vinavyotawala mara nyingi katika eneo la Kivu Kusini.
Kifo cha Daktari Muzima Rushombo André, mwana wa Mheshimiwa Muzima wa Muzima, kiongozi mkubwa na chifu wa jadi wa Chefferie ya Bafuliru, kimechukuliwa kama jambo linalopaswa kufuatiliwa kwa karibu. Jamii Mpya ya Kiraia imesisitiza kuwa ushuhuda wote muhimu unapaswa kukusanywa ili kifo hiki kisielekezwe tu kama bahati mbaya bali kueleweka katika muktadha wa rivalité na wivu vinavyoendelea kugubika jamii ya eneo letu.
Kwa maneno yake ya mwisho, Jamii Mpya ya Kiraia ya Kongo imetoa wito kwa mamlaka husika kuhakikisha ukweli unajulikana na haki ipatikane.























