Kwa mujibu wa ushuhuda mbalimbali uliokusanywa na SOS Médias Burundi, milio ya silaha nzito na nyepesi inaendelea kusilika katika baadhi ya mitaa ya jiji, jambo linalosababisha hofu na woga miongoni mwa wakazi.
Kutokana na kuongezeka kwa mvutano huo, baadhi ya wakazi wameanza kuondoka majumbani mwao wakihofia kuzorota kwa haraka kwa hali ya usalama.
Vyanzo vya ndani vinaeleza kuwa milipuko hiyo inaripotiwa kutokea karibu na kambi za kijeshi za Musaga, kusini mwa jiji (Bujumbura).
Chanzo kimoja cha kiusalama kimeeleza pia uwezekano wa matumizi ya “mabomu”, ingawa taarifa hiyo bado haijathibitishwa rasmi.






















